KAMISHENI YA KISWAHILI YA AFRIKA MASHARIKI NA HATIMA YA VISWAHILI SANIFU

Authors

  • Gervas A. Kawonga Author

DOI:

https://doi.org/10.2023/t4kw9y83

Abstract

Makala haya yanahusu nafasi ya Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (KAKAMA) ikiwa ni tumaini jipya katika kudhibiti Viswahili sanifu katika nchi za Afrika Mashariki. Makala haya ni matokeo ya utafiti wa maktabani uliohakiki maandiko mbalimbali. Hoja kuu ya makala haya ni kwamba wakati wa ukoloni kulikuwa na Kiswahili sanifu cha Afrika Mashariki ambacho hakipo katika Afrika Mashariki huru. Hii ni kwa sababu, baada ya uhuru, Kamati ya Lugha (Kiswahili) ya Afrika Mashariki ilisambaratika na huo ukawa mwanzo wa kuibuka na kukua kwa Viswahili sanifu vya kimaeneo. Kuundwa kwa BAKITA Tanzania Bara na BAKIZA kwa upande wa Zanzibar kuliimarisha launi za Kiswahili. Pia, kutungwa kwa kamusi za KKS, KKF na KTK kwa Tanzania, Zanzibar na Kenya mtawalia ni ushahidi wa kuimarika kwa Viswahili sanifu vya kimaeneo. Vichocheo vya kuinukia kwa Viswahili hivyo vinaweza kuwa vingi lakini mawanda ya kisiasa kama kipengele muhimu cha ikolojia ya lugha yana nafasi ya juu zaidi kuliko sababu kuntu za kitaaluma. Hitimisho la makala haya ni kwamba inafaa kuwe na usanifishaji mpya na endelevu wa Kiswahili ili kurejesha umoja wa lugha wa Afrika Mashariki uliokuwapo wakati wa ukoloni. Wito wa makala haya ni kwamba KAKAMA inapaswa kuchukua hatua zinazostahiki kusitisha ongezeko la Viswahili sanifu kwa madai ya uhuru wa jamii kutumia lugha itakavyo. Muhuri wa ithibati lazima urejeshwe kwa KAKAMA ili kuhakikisha kwamba msamiati, miundo na matumizi ya Kiswahili sanifu kwa jumla yanasawazishwa. Matumizi rasmi ya lugha kama vile katika elimu na utawala yanapaswa kuwa yale yaliyokubaliwa na watumiaji kwa vigezo vya pamoja.

Downloads

Download data is not yet available.

Published

2025-01-22

How to Cite

Kawonga, G. A. (2025). KAMISHENI YA KISWAHILI YA AFRIKA MASHARIKI NA HATIMA YA VISWAHILI SANIFU. JARIDA LA CHAUKIDU, 16-28. https://doi.org/10.2023/t4kw9y83