NAFASI YA KISWAHILI KATIKA UFASIRI WAMIKATABA, SHERIA ZA KITAIFA, NAKIMATAIFA NCHINI KENYA
DOI:
https://doi.org/10.2023/6m8v5t27Muhtasari
Kikwazo cha lugha katika ufahamu wa masuala nyeti ya kitaifa au hata kimataifa huweza kuharibu mawasiliano nchini na kusababisha kutoelewana miongoni mwa watu. Aidha, kikwazo hicho kinaweza kukwamisha juhudi za maendeleo katika taifa au hata kuzuia wananchi kuelewa yale yanayojiri katika nyanja za kimataifa. Kikwazo hiki hutokea pale ambapo lugha moja rasmi ndiyo inayotumiwa hata kama kuna lugha mbili rasmi, kuunda sera za nchi, kufafanulia mikataba na makubaliano ya kitaifa na kimataifa au hata kuelezea sheria za nchi. Nchini Kenya, wananchi wengi hawafahamu sera za nchi au hata Katiba ya Kenya. Hii ni kutokana na hali kwamba Kiingereza ndicho kinachotumiwa kuunda sera, kuandikia Katiba ya nchi, mbali na kuhifadhi mikataba na makubaliano yoyote rasmi yawe ni ya kitaifa au kimataifa. Je, nafasi ya Kiswahili katika kuwafahamisha wananchi yale yanayojiri nchini mwao iko wapi? Makala yanajadili kikwazo cha lugha katika ufahamu wa masuala nyeti, sera au hata miradi ya kitaifa au kimataifa inayotekelezwa nchini na jinsi masuala hayo yanavyoathiri wananchi walio wengi. Udurusu wa baadhi ya mikataba, sera, sheria na makubaliano ya kitaifa na kimataifa umefanywa ili kuonesha jinsi yasivyoeleweka au kufahamika miongoni mwa Wakenya wengi. Makala yanapendekeza mikakati ya kuzingatiwa ili kuwahusisha wananchi wote kama washiriki katika mambo yanayowaathiri na kuweza kuchangia katika mijadala ya kitaifa na kimataifa inayoathiri maisha yao.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode