RUWAZA YA SHUJAA YA CAMPBEL
TOFAUTI ZINAZOONESHWA NA NGANO TEULE ZA KIEWE KUTOKA GHANA
DOI:
https://doi.org/10.2023/fefc1937Muhtasari
Ngano ni sanaa ya usimulizi ya Kiewe ambapo usimulizi, utendaji na ubunifu zinaungana pamoja katika mfumo wa kifasihi na mtu mmoja au kundi la watu. Tunasema mtu mmoja kwa maana ya kuwa baadhi ya mbinu zinazotumika zinategemea uwezo wa kifasihi wa msimulizi. Vilevile, zinaweza kuwa kwa kundi la wasimulizi kwa sababu baadhi ya mbinu zinazotumika ni kutoka katika jamii na zinagunduliwa pamoja na jamii. Utanzu wa ngano (ambao kwa Kiewe ni Gli) huchukuliwa na Waewe kuwa ni usimulizi wa mdomo unaotumia mbinu za kifasihi za kuwakilisha tamaduni na maisha ya jamii hiyo. Kumbo hii ya fasihi simulizi inatumika kuelimisha jamii ambayo inakuwa katika mfumo wa kuchanganya maadili, mafunzo na burudani kwa pamoja. Maudhui muhimu katika Gli ni kukemea tabia mbaya, ambayo haikubaliki katika jamii, na kuhimiza tabia njema, zinazokubalika katika jamii inayohusika. Hali kadhalika, ngano hutumika kuwatia moyo wanajamii katika shida na matatizo mbalimbali. Ngano nyingi hutumia mbinu mbalimbali za kifani katika uwasilishaji wa maudhui yake. Miongoni mwa mbinu maarufu zinazotumiwa na ngano ni matumizi ya motifu, na hasa motifu ya safari ya msako. Motifu hii hutumiwa kuwahamasisha wanajamii kujitafutia maisha mazuri kupitia safari ya msako. Aidha, hutumika kuibua maadili mbalimbali muhimu kwa jamii hii. Katika makala haya, tunajaribu kuwasilisha namna ngano za Kiewe zinavyoonesha utofauti katika ruwaza ya shujaa kwa mujibu wa Campbel. Kwa kuzungumzia suala hili, makala haya yamezingatia masimulizi ya ngano za Kiewe yenye motifu ya safari ya msako.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode