UCHANGANUZI WA MWINGILIANO WA MANENO KATIKA MAZUNGUMZO KWA KISWAHILI MIONGONI MWA WANAFUNZI WA SHULE YA UPILI UGANDA
DOI:
https://doi.org/10.2023/ayp4tf42Muhtasari
Lugha huingiliana na kuathiriana zaidi zinapotumiwa katika mazungumzo katika eneo mahususi la kijiografia. Mwingiliano wa lugha hujitokea katika viwango anuwai vya kiisimu mojawapo ikiwa mwingiliano wa maneno kati ya L1 na L2. Makala haya yameshughulikia matokeo ya utafiti kuhusu uchanganuzi wa mwingiliano wa maneno katika mazungumzo kwa Kiswahili kati ya lugha ya Kigisu na Kiswahili nchini Uganda. Utafiti huu ulitokana na tafiti za hapo awali zinazoripoti kwamba lugha ya kwanza huathiri umilisi wa lugha ya pili katika nyanja mbalimbali za kiisimu. Kwa hiyo, makala haya yanaripoti kuhusu matokeo ya matumizi ya maneno ya vitenzi na nomino miongoni mwa wanafunzi wanaojifunza na kuzungumza Kiswahili kama lugha ya pili ili kubainisha jinsi lugha ya Kigisu inavyoathiri lugha ya mazungumzo kwa Kiswahili miongoni mwa wanafunzi wa shule za upili kama lugha ya pili. Nadharia za Mwingiliano Lugha ya Selinker (1972), na Uchanganuzi Makosa kama inavyoelezwa na Lennon (2008) zilitumika kubainisha athari za mwingiliano wa maneno kati ya L1 na L2. Data ilikusanywa kutoka kwa wanafunzi 78 wa kidato cha tatu miongoni mwa wanafunzi wa shule nne za upili wanaoongea Kigisu kama L1 na ambao ni wanafunzi wa lugha ya Kiswahili. Matokea ya utafiti yanadhihirisha ujumuishaji wa nomino na vitenzi katika mazungumzo kwa Kiswahili, uhamishaji wa nomino na vitenzi kutoka L1 kwa L2 na ubadilishanaji wa nomino na vitenzi vya Kiswahili na vile vya Kigisu katika mazungumzo.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode