LUGHA YA KIDIJITALI KAMA LUGHA YA KIMAZUNGUMZOANDISHI: MFANO WA MAWASILIANO YA FACEBOOK

Waandishi

  • Toboso Mahero Bernard ##default.groups.name.author##
  • Mosol Kandagor ##default.groups.name.author##
  • Allan Opijah ##default.groups.name.author##

DOI:

https://doi.org/10.2023/g45gy352

Muhtasari

Mitandao mingi ya kijamii imeibuka miaka ya hivi karibuni. Kuzuka kwa mitandao hii kumesababisha mabadiliko makubwa katika lugha, mitindo ya mawasiliano na mchakato wa mawasiliano. Mawasiliano ya kilugha yamegawika katika tanzu kuu mbili; yaani mawasiliano ya kimaandishi na yale yakimazungumzo. Kila utanzu wa mawasiliano ya kilugha una sifa zake bainifu. Kwa hivyo, lugha ya kimaandishi ni tofauti kisifa na lugha ya kimazungumzo. Hata hivyo, kuzuka kwa mitandao ya kijamii kumezua lugha ya kidijitali yenye mitindo ibuka inayodhihirisha sifa mseto za mawasiliano ya kimaandishi ya yale ya kimazungumzo. Utafiti huu unachunguza lugha ya kidijitali katika Facebook na kusisitiza kwamba ni lugha ya mazungumzo andishi.

Downloads

Download data is not yet available.

Imechapishwa

2025-01-22

Jinsi ya Kunukuu

Bernard, T. M. ., Mosol Kandagor, & Opijah, A. (2025). LUGHA YA KIDIJITALI KAMA LUGHA YA KIMAZUNGUMZOANDISHI: MFANO WA MAWASILIANO YA FACEBOOK. JARIDA LA CHAUKIDU, 259-267. https://doi.org/10.2023/g45gy352