UNAFIKI WA VIONGOZI WA KISIASA KAMA MKAKATI WA KUWAWEKA MAMLAKANI: MFANO KUTOKA RIWAYA ZA KATAMA MKANGI: MAFUTA NA WALENISI
DOI:
https://doi.org/10.2023/7ykkej30Muhtasari
Makala haya yanaangazia usawiri wa unafiki wa viongozi wa kisiasa kama mkakati wa kuwaweka mamlakani katika riwaya za Katama Mkangi Mafuta na Walenisi. Riwaya zote mbili ni za kiitikadi. Zinachunguza jinsi mfumo wa kisiasa unaodhibitiwa na tabaka la wachache unavyoweza kuathiri maisha ya wanaotawaliwa kisiasa. Riwaya hizi zinaonesha uovu uliopo katika tawala ambazo hazitilii maanani masilahi ya wanyonge. Ni kielelezo cha jinsi jamii inavyoweza kujinasua kutoka katika mfumo unaowakandamiza na unaowadhalilisha wengi. Mkangi amesawiri viongozi dhalimu wa kibepari wanaojiweka na kujisetiri mamlakani kupitia unafiki. Makala haya yanadhamiria kusawiri madhila wanayotendewa wanajamii na viongozi dhalimu wasiowajali kupitia unafiki ambao wameufanya kuwa ukweli. Kilele cha uozo wa viongozi wa kisiasa kinajitokeza wakati ambapo uhuru wa kuongea unadhibitiwa na yeyote anayepatikana na ‘hatia’ hii anahukumiwa kifo au anapata adhabu ya kufutwa kazi pasipo na sababu yenye mashiko. Jitihada za wanyonge za kukata silisili za udhalimu zinabainika wanapoamua kupindua mfumo huu wa kisiasa kwa kuwatimua viongozi dhalimu na wanafiki kupitia mapinduzi. Umuhimu wa makala haya ni kubainisha kuwa kupitia kazi za sanaa, hasa fasihi andishi, msomaji anaweza kubaini hali halisi ya maisha yake na wakati huohuo kupata suluhu ya kutatua matatizo yanayomkumba na jamii yake.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode