JAZANDA YA MAJINA YA MAONESHO KATIKA TAMTHILIA ZA KISWAHILI: MIFANO YA TAMTHILIYA ZA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE NA CHANZO NI WEWE
MIFANO YA TAMTHILIYA ZA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE NA CHANZO NI WEWE
DOI:
https://doi.org/10.2023/rg4z2q28Muhtasari
Makala haya yanahusu jazanda ya majina ya maonesho katika tamthiliya za Kiswahili: huku mifano ikitolewa kutoka tamthilia za Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe ya E. Semzaba na Chanzo ni Wewe ya W. Himu. Makala yanachambua jinsi jazanda zilizotumika kubuni majina ya maonesho zinavyosaidia kudokeza mawazo ya msingi katika onesho husika. Mjadala unajikita kuonesha namna watunzi hao walivyoepuka majina zoefu ya maonesho ambayo pengine ni majina ya kimapokeo. Tamthiliya nyingi hutumia majina kama vile onyesho, kitendo, sehemu n.k. Watunzi hawa wamekuwa wabunifu kwa kukiuka kaida fulani zilizozoeleka na kutoa majina yenye kutafakarisha zaidi. Mwisho, makala yanaonesha jinsi jazanda za majina ya maonesho katika tamthiliya teule zinavyoakisi migongano ya wahusika ndani ya maonesho ya tamthilia hizo. Uakisi huo unajibainisha katika mfuatano, muendelezano na mkamilishano wa matukio, vitendo na maonyesho ndani ya tamthiliya hizo. Nadharia ya Usasa ndiyo mwongozo wa ufafanuzi wa makala haya. Nadharia hii hutumiwa kuzielezea au kuzitambulisha sifa mpya za dhamira, tanzu, dhana na mitindo ya kifasihi inayojitenga na misingi na jadi ya sanaa na utamaduni wa Kimagharibi au uliokuwapo.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode