MATUMIZI YA FASIHI SIMULIZI KATIKA KAMPENI ZA UCHAGUZI TANZANIA: TATHMINI YA DHIMA YA NYIMBO
TATHMINI YA DHIMA YA NYIMBO
DOI:
https://doi.org/10.2023/g837nb36Muhtasari
Fasihi simulizi kama chombo cha kazi cha jamii haiwezi kujitenga na jamii katika shughuli zake kama vile za kiuchumi, kiutamaduni, kijamii, na kisiasa. Makala haya yanaeleza matumizi ya fasihi simulizi katika kampeni za siasa nchini Tanzania kwa kutumia kipengele cha nyimbo. Makala yanaeleza kuwa nyimbo ni nyenzo mojawapo inayotumika katika michakato ya kisiasa ikiwa ni pamoja na mikutano ya kampeni za uchaguzi. Data za makala haya zinazotokana na nyimbo za kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 zilizotumika kueleza falsafa, sera, dira, na matarajio ya wanasiasa katika ugombea wao wa nafasi za uongozi wa kisiasa. Kwa kutumia Nadharia ya Uhalisia wa Urasimi, makala haya yanaonesha kuwa nyimbo za kampeni za uchaguzi zinatumika kueleza ukweli wa mambo bila kutia chuku. Nyimbo hizi ziznaeleza mambo dhahiri ya kila siku na yanayoweza kuthibitika. Makala haya yanaeleza kuwa mbinu ya matumizi ya nyimbo katika kampeni za kisiasa za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015, na bila shaka katika kampeni zilizotangulia na zile zitakazokuja baadaye, ilitumika kipragmatiki kwa minajili ya kufikia matarajio ya kisiasa ya makundi ya wanasiasa na vyama vya siasa kwa ujumla. Kwa upande mmoja, mbinu hiyo ilikuwa na lengo la kutengeneza hadhara za wapiga kura na kuiweka tayari kwa ajili ya kusikiliza kampeni na hatimaye baadaye kupiga kura. Hali kadhalika, ilikuwa na azma ya kueleza na kusifu sera na falsafa za wagombea na vyama vyao vya siasa. Vilevile, ilikuwa ni mbinu ya kupinga sera na falsafa ya wagombea na vyama vingine. Katika makala haya, inaelezwa kuwa, pamoja na malengo hayo, lengo kuu kupita yote la kutumia mbinu ya nyimbo, kama kipengele cha fasihi simulizi, ilikuwa hatimaye kupata ushindi katika uchaguzi wenyewe.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode