MITAZAMO YA LUGHA NA ELIMU KATIKA JAMII ZA AFRIKA MASHARIKI
DOI:
https://doi.org/10.2023/hf8v8k13Muhtasari
Nchi nyingi za Afrika Mashariki na barani Afrika zimejaliwa kuwa na idadi kubwa za lugha. Ni jambo la kawaida kukuta lugha zaidi ya mia moja zinazozungumzwa katika nchi moja pekee. Hali hii imeleta utata na hata kusababisha baadhi ya lugha kukosa wasemaji (Brock-Utne na wenzie, 2010). Kiswahili, lugha ya taifa nchini Kenya na Tanzania ni mojawapo ya lugha zinazokabiliwa na utata mkubwa hasa kuhusu matumizi yake kama lugha ya kufundishia au kufundishwa katika mifumo ya elimu. Huku wadau wengi wa lugha wakihimiza matumizi ya lugha itakayomwezesha mwanafunzi kujifunza na kuyaelewa mazingira yake, bado kuna athari kubwa katika kukabiliana na ulimwengu wa utandawazi. Makala haya yanakusudia kuchambua kwa undani zaidi mitazamo ya lugha katika Afrika ya Mashariki (nchi za Kenya na Tanzania) na kulinganua mitazamo ya lugha na umuhimu wake katika kupiga vita dhidi ya kasumba ya kikoloni na utumwa wa Kiingereza. Ingawa tafiti nyingi zimeeleza zaidi kuhusu sera za lugha katika nchi hizi, makala haya yanatoa hoja kuwa mitazamo ya lugha imeathiriwa sana na sera hizo za lugha na zaidi pia mambo mengine kama ubeberu wa kiisimu na utandawazi. Hivyo basi, tutachunguza jinsi makala na tafiti mbalimbali katika nchi hizi mbili, zilivyozungumzia masuala haya tangu wakati wa ukoloni hadi miaka ya karibuni na iwapo kumekuwa na mabadiliko yoyote.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode