DHIMA NA CHANGAMOTO ZA MATUMIZI YA TAFSIRI KATIKA UFUNDISHAJI WA KISWAHILI NCHINI UGANDA
DOI:
https://doi.org/10.2023/bak38m84Muhtasari
Ufundishaji wa lugha ya kigeni au lugha ya pili kwa wanafunzi wenye umilisi wa lugha na desturi zao si jambo rahisi. Wakati mwingine, walimu hutumia tafsiri ili wanafunzi waweze kuelewa vipengele vya lugha ya kigeni inayofundishwa. Makala haya yanaangazia matumizi ya mbinu ya tafsiri katika shule za sekondari jijini Kampala nchini Uganda. Lengo la makala haya ni kujadili iwapo tafsiri inaweza kutambuliwa kama stadi ya tano katika ufundishaji wa Kiswahili kwa wageni. Utafiti huu umechochewa na mkanganyiko uliopo kuhusu nafasi ya tafsiri katika ufundishaji wa lugha. Ingawa tafsiri hutumiwa katika ufundishaji wa Kiswahili kama lugha ya kigeni, mbinu hii haibainishwi kama mbinu mojawapo ya ufundishaji kwenye mitaala. Data za utafiti ni za uwandani na maktabani. Data za uwandani zilikusanywa kwa njia ya ushuhudiaji, hojaji na uchambuzi wa nyaraka. Matokeo yanaonesha kwamba tafsiri ni mbinu inayotumiwa kwa upana katika ufundishaji wa Kiswahili nchini Uganda. Halikadhalika, makala haya yamebainisha kuwa Kiswahili ni lugha ya kigeni nchini Uganda, hali inayowafanya walimu kutegemea tafsiri baina ya Kiswahili na Kiingereza. Kwa kuhitimisha, makala haya yanashadidia kwamba hata kama tafsiri ina changamoto zake katika ufundishaji wa lugha za kigeni, haiwezi kukwepeka katika ufundishaji wa Kiswahili katika mazingira ambamo lugha hii haitumiwi katika mawasiliano ya kila siku.
Downloads
Imechapishwa
Toleo
Sehemu
Leseni
Hakimiliki (c) 2025 JARIDA LA CHAUKIDU

Kazi hii imewekwa chini ya Leseni ya Creative Commons Kutambulisha-Isiyo ya Kibiashara 4.0 Kimataifa.
Masharti ya Leseni Chini ya CC Attribution-NonCommercial 4.0 (CC BY-NC 4.0)
1. Wigo wa Matumizi
Wasomaji wanaonunua upatikanaji wa makala za jarida wanaruhusiwa kufanya yafuatayo:
- Kusoma: Kupata na kuona maudhui kwa matumizi ya kibinafsi.
- Kushiriki: Kusambaza makala zilizopatikana kwa njia zisizo za kibiashara, kwa mfano, na wenzako kwa madhumuni ya kielimu au utafiti.
- Kubadilisha: Kuunda kazi zitokanazo (kwa mfano, muhtasari au marekebisho) kwa madhumuni yasiyo ya kibiashara.
2. Masharti ya Matumizi
Utoaji wa Sifa:
- Utambuzi sahihi lazima zitolewe kwa mwandishi/wandishi na jarida wakati wa kusambaza au kubadilisha maudhui.
- Utambuzi unapaswa kujumuisha jina la mwandishi/wandishi, kichwa cha makala, jina la jarida, toleo/matoleo, na kiungo cha jarida au DOI ya makala.
- Mabadiliko yoyote yaliyofanywa kwa kazi lazima yaonyeshwe wazi na kufanyiwa utambuzi ipasavyo.
Kutotumika Kibiashara:
- Makala hayawezi kutumiwa kwa madhumuni ya kibiashara, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu kuuza tena, kusambaza kwa faida, au kuingizwa kwenye bidhaa au huduma za kibiashara.
- Matumizi ya kitaasisi (kwa mfano, kwa mafunzo au warsha) lazima yaambatane na masharti yasiyo ya kibiashara isipokuwa ruhusa ya wazi imetolewa na jarida.
3. Vizuizi vya Upatikanaji na Kushiriki
- Upatikanaji wa Kulipia: Upatikanaji wa makala za jarida unahusiana tu na waliojisajili au watu binafsi waliolipia makala. Usambazaji au kushiriki makala kamili bila ruhusa unakatazwa.
- Hakuna Vizuizi vya Ziada: Wasomaji hawaruhusiwi kuongeza vikwazo vya kisheria au kiteknolojia ambavyo vinazuia wengine kutumia maudhui kama ilivyoainishwa na leseni hii.
4. Matumizi Yanayokatazwa
Makala hayawezi:
- Kusambazwa kwenye majukwaa ya kibiashara bila ruhusa ya wazi.
- Kutumika katika shughuli zinazozalisha faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja (kwa mfano, kama sehemu ya kozi au matukio ya kulipiwa) bila idhini ya awali kutoka kwa jarida.
- Kubadilishwa kwa madhumuni yanayoweza kupotosha maana ya awali ya kazi.
5. Kanusho
- Maudhui yametolewa “kama yalivyo,” bila dhamana au uhakikisho wowote kutoka kwa waandishi au jarida.
- Waandishi wala jarida hawatawajibika kwa madai yoyote, madhara, au matatizo yanayojitokeza kutokana na matumizi ya makala.
6. Maelezo ya Ziada
- Kwa Wasomaji: Maudhui yaliyonunuliwa ni kwa matumizi ya kibinafsi, kielimu, au ya utafiti pekee, kwa kuzingatia masharti yasiyo ya kibiashara na utoaji wa sifa.
- Kwa Taasisi: Taasisi zinazonunua upatikanaji wa pamoja au usajili lazima zihakikishe kuwa upatikanaji unahusiana tu na watumiaji waliosajiliwa na unazingatia masharti yasiyo ya kibiashara.
Kwa maandishi kamili ya leseni ya CC BY-NC 4.0, tembelea:
https://creativecommons.org/licenses/by-nc/4.0/legalcode