Jarida la CHAUKIDU

Current Issue

2023
Published October 13, 2023
Dira ya Karne ya 21 Ukuaji wa Kiswahili Na Ustawi wa Jamii

Tunasikitika kwamba toleo hili la CHAUKIDU halikuweza kutoka kwa wakati uliotarajiwa kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Tunajua kwamba ni toleo lililosubiriwa na wengi kwa hamu kubwa. Kwa hivyo, tunawaomba wadau wetu wote wakiwemo waandishi wa makala na wasomaji watuwie radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza. Ushirikiano wa wataalamu kutoka maeneo mbalimbali ya dunia ni muhimu kwa taaluma za Kiswahili ambazo zinachangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa lugha ya Kiswahili na kuenea kwake duniani. Katika Kongamano lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mwishoni mwa mwaka wa 2017, wadau kutoka sekta mbalimbali walishiriki na kujadili mchango wa kila tasnia katika kukiendeleza na kukiimarisha Kiswahili. Kongamano lilijadili jinsi kila tasnia ilivyochangia na inavyoendelea kuchangia kwa namna tofautitofauti ukuzaji wa lugha ya Kiswahili na jinsi ambavyo Kiswahili kilichangia na kinaendelea kuchangia kustawisha tasnia husika. Mawasilisho, mazungumzo, na mijadala iliyofanyika iliwasaidia washiriki kuanza kutafakari juu ya uundaji wa dira ya ukuzaji endelevu wa Kiswahili na ustawi endelevu wa jamii katika karne ya 21 kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Matokeo ya mijadala yote hiyo ni toleo hili la pili la CHAUKIDU ambalo linajumuisha mawazo ya wadau mbalimbali kupitia mawasilisho yaliyoangazia vipengele mbalimbali kama vile fasihi, isimu, nafasi ya vyombo vya habari katika ukuaji wa Kiswahili na ufunzaji na ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili. Katika toleo hili, mada mbalimbali zimeshughulikiwa na waandishi kutokana na tafiti zao za uwandani na mapitio ya maandishi maktabani na kwingineko. Kimsingi basi, kuna makala mengi ambayo yamechapishwa katika toleo hili kuchangia hazina kubwa ya lugha ya Kiswahili. Kazi zilizochapashwa katika toleo hili ni zile zilizoitikia mwito wa mada kuu ya mkusanyiko wa wataalamu mbalimbali kuhusu Dira ya Karne ya 21– Ukuaji wa Kiswahili na Ustawi wa Jamii.

Makala za Makongamano

Leonard Muaka, Mahiri Mwita, Beatrice Mkenda, Charles Bwenge (Author)
0-xii
Front Matter
Requires Subscription Front Matter pdf (Swahili)
Clara Momanyi (Author)
1-15
NAFASI YA KISWAHILI KATIKA UFASIRI WA MIKATABA, SHERIA ZA KITAIFA, NA KIMATAIFA NCHINI KENYA
Requires Subscription Momanyi PDF
Gervas Kawonga (Author)
16-28
Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki na Hatima ya Viswahili Sanifu
Requires Subscription Kawonga PDF
Iribe Mwangi (Author)
29-39
KISWAHILI KAMA LUGHA RASMI NA LINGUA FRANKA YA AFRIKA MASHARIKI: JE, NI BARAKA AU NI LAANA?
Requires Subscription Iribemwangi PDF (Swahili)
Leah Y. Kiloba, Getruda E. Shima (Author)
40-58
JAZANDA YA MAJINA YA MAONESHO KATIKA TAMTHILIA ZA KISWAHILI: MIFANO YA TAMTHILIYA ZA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE NA CHANZO NI WEWE
Requires Subscription Kiloba PDF (Swahili)
Aneth Kasebele (Author)
59-69
MABADILIKO YA KIJAMII NA USAWIRI WA MWANAMKE: UCHAMBUZI WA WIMBO WA TAARABU WA ISHA RAMADHANI.
Requires Subscription Kasebele PDF (Swahili)
Hadija Jilala (Author)
70-86
TAFSIRI BINAFSI KATIKA NADHARIA YA TAFSIRI: UTHABITI, CHANGAMOTO NA MAPENDEKEZO
Requires Subscription Jilala PDF (Swahili)
Sarah Ndanu M. Ngesu, Leonard Muaka (Author)
87-109
DHIMA NA CHANGAMOTO ZA MATUMIZI YA TAFSIRI KATIKA UFUNDISHAJI WA KISWAHILI NCHINI UGANDA
Requires Subscription Ngesu et al. PDF (Swahili)
Fokas Nchimbi (Author)
111-120
MATUMIZI YA FASIHI SIMULIZI KATIKA KAMPENI ZA UCHAGUZI TANZANIA: TATHMINI YA DHIMA YA NYIMBO
Requires Subscription Nchimbi PDF (Swahili)
Rose Jackson Mbijima (Author)
121-135
MATUMIZI YA LUGHA KATIKA RIWAYA YA KWANZA YA KISWAHILI YA UHURU WA WATUMWA NA RIWAYA YA KWANZA YA KISWAHILI YA MAJARIBIO YA NAGONA
Requires Subscription Mbijima PDF (Swahili)
Anne Jebet, Beatrice Mkenda (Author)
126-149
MITAZAMO YA LUGHA NA ELIMU KATIKA JAMII ZA AFRIKA MASHARIKI
Requires Subscription Jebet et al. PDF (Swahili)
Issaya Lupogo (Author)
150-160
MZUNGUKO WA UKANUSHI WA JESPERSEN KATIKA LUGHA YA KISWAHILI
Requires Subscription Lupogo PDF (Swahili)
Justus Kyalo Muusya, Leah W. Mwangi (Author)
161-173
MWINGILIANOMATINI KATIKA USAWIRI WA MWANAMKE KATI YA TAMTHILIA ZA KILIO CHA HAKI YA A. MAZRUI NA KIGOGO YA P. KEA
Requires Subscription Muusya et al. PDF (Swahili)
Felix Sosoo (Author)
174-197
RUWAZA YA SHUJAA YA CAMPBEL: TOFAUTI ZINAZOONESHWA NA NGANO TEULE ZA KIEWE KUTOKA GHANA
Requires Subscription FelixSosoo PDF (Swahili)
Sebastian Nyerere Mbwillow (Author)
198-205
HADHI YA TONI YA KIKINGA
Requires Subscription Mbwillow PDF (Swahili)
Rosanna Tramutoli (Author)
206-219
‘HURUMA ILIGEUKA MVUKE’: UCHAMBUZI WA SITIARI ZA HISIA KATIKA KAZI ZA FASIHI YA KISWAHILI
Requires Subscription Tramutoli PDF (Swahili)
Ahmad Sovu (Author)
220-228
MOFIMU SABABISHI -Z- KATIKA KITENZI CHA KISWAHILI
Requires Subscription Sovu PDF (Swahili)
Stephen J. Maina (Author)
229-235
KITOVU CHA KISWAHILI (SWAHILI HUB)
Requires Subscription Maina PDF (Swahili)
James Marwa Mwita (Author)
236-245
TATHMINI YA MCHANGO WA VYOMBO VYA HABARI VYA KICHINA KATIKA KUKUZA NA KUENEZA KISWAHILI
Requires Subscription Mwita PDF (Swahili)
Mulei Martin (Author)
UCHANGANUZI WA MWINGILIANO WA MANENO KATIKA MAZUNGUMZO KWA KISWAHILI MIONGONI MWA WANAFUNZI WA SHULE YA UPILI UGANDA
Requires Subscription Martin PDF (Swahili)
Toboso Mahero Bernard, Mosol Kandagor, Allan Opijah (Author)
259-267
LUGHA YA KIDIJITALI KAMA LUGHA YA KIMAZUNGUMZOANDISHI: MFANO WA MAWASILIANO YA FACEBOOK
Requires Subscription Benard et al. PDF (Swahili)
Naomi Musembi (Author)
268-291
UNAFIKI WA VIONGOZI WA KISIASA KAMA MKAKATI WA KUWAWEKA MAMLAKANI: MFANO KUTOKA RIWAYA ZA KATAMA MKANGI: MAFUTA NA WALENISI
Requires Subscription Musembi PDF (Swahili)
View All Issues